WATU WENYE KUTOSHEREZA

David Wilkerson (1931-2011)

Mtume Paulo aliandika, "Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi ni watoto wa Mungu" (Warumi 8:16). Maneno "watoto wa Mungu" mara nyingi hutumiwa kwa kuelezea waumini, lakini maneno yanaweza kutumiwa pia kwa uhakika, kwa ufahamu mdogo wa nguvu na kina cha maana yake ya kweli.

Kuwa mtoto wa Mungu inamaanisha tu kuwa mtegemezi wa Mungu; yaani, "asiyeweza kuwepo au kufanya kazi bila msaada kutoka kwa Mungu." Mtoto wa Mungu anajua hawezi kudhibiti maisha yake bila msaada wa kila siku wa Bwana.

Wengi wenye dhambi ni watu wenye kujitegemea ambao wanajiona kama wenye mafanikio makubwa –watu wanaoweza. Wanashuhudia kwamba chochote kile akili inaweza kufikiri, kinawezakana  kufikia - kwamba kwa mtazamo wa akili sahihi, mtu anaweza kufanya kitu chochote.

Kanisa limejazwa na vitabu vya kila aina, vingi vinahusu kushinda ushindi wako mwenyewe juu ya kuwa mwenyewe, shaka, hofu na upweke. Wengi katika kanisa wanaamini ikiwa una fomu sahihi, unaweza kujitambua kila kitu na kutatua matatizo yako mwenyewe. Mtazamo huu unasema, "Mungu, umenipa akili njema nitafikiri tu kupitia hii na kulitenda."

Wakati mmoja Yesu aliwaona wanafunzi wake wakiongea kati yao kuhusu nani atakayekuwa mkuu zaidi katika ufalme wa Mungu na akawapa somo. "Yesu akamwita mtoto mdogo, akamtiya katikati yao, akasema, amin, nawambia, musipoongoka na kuwa kama watoto wadogo, hamtaingia katika ufalme wa mbinguni" (Mathayo 18:2-3).

Yesu alikuwa akisema, "Sahabu juu ya yule atakaye kuwa mkuu zaidi. Unapaswa kufikiri tena uhusiano wako kwangu na kujifunza jinsi ya kutembea katika maisha haya." Mtoto huyu aliwakilisha maisha ya utegemezi wa jumla, kwa sababu watoto hawawezi kujitunza wenyewe.

Je! Umejifunza kuwa mtegemezi kabisa kwa uongozi wa Roho Mtakatifu? Njoo kwake kama mtoto mdogo na atakuwa na mapinduzi ya kufikiri kwako!