PUMZIKA KATIKA UPENDO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Je! Unaamini kama imani yako ni dhaifu? Je! Umeomba kwa bidii juu ya haja na kumwamini Mungu kwa moyo wako wote kwamba ataweza kutoa, na hukuona jibu? Unasoma ahadi za utukufu juu ya vitu vyote vinavyowezekana kwa wale wanaoamini: "Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea" (Mathayo 21:22). "Yo yote myaombayo wakati mkisali, amini ya kwamba mnayapokea, nayo yatukuwa yenu" (Marko 11:24). Na ulidai ahadi hizo! Hata hivyo, jaribu kama unavyoweza kuamini - kwa kweli, unaamini kweli - mara nyingi huachwa umechanganyikiwa, kwa sababu jibu limechelewa au haliko kwenye mtazamo.

Wengine wanaamini kwamba kuna sababu mbili tu ambazo hukupata kile ulichoombea: ama imani yako inakasoro au kuna dhambi katika maisha yako. Umefanywa kuwa Mungu anapaswa kushikilia jibu mpaka imani yako iweze kuongezeka ili imlizishe. Au ubora wa imani yako haukuja kwa vigezo vya Mungu kuhusu maombi yenye kujibiwa, au labda umesema maneno mabaya au "kukiri kubaya."

Rafiki yangu, aina hiyo ya theologia ni udanganyifu na ni kofe kwenye uso wa Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo. Mungu anafanya miujiza kwa kujibu maombi ya Imani, na ahadi zote katika Neno la Mungu ni kweli. Lakini kuna jambo la ajabu kuhusu jinsi Mungu anavyofanya. Yeye hana motisha wa kututenda kwa sababu ya imani yetu pekee. Mungu ni upendo, na hili ndiyo ndilo linamchochea kutenda.

"Hata kama sisi hatuamini, anaendelea kuwa mwaminifu kwetu na atatusaidia, kwa maana hawezi kutukana sisi ambao ni sehemu yake mwenyewe, naye atatimiza daima ahadi zake" (2 Timotheo 2:13, TLB). Imani yangu, imani yako, imani zote zinapaswa kupumzika juu ya fadhili za upendo na maozi ya Baba wetu wa mbinguni.

"Bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijuwa, ya kuwa mimi ni Bwana anayefanya fadhili zenye upendo, hukumu, na haki katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo" (Yeremia 9:24). Hebu tujisifu katika upendo mkali na wema wa Baba yetu leo.