JIA PEKEE YA KUZAA MATUNDA
Matunda katika Biblia yanaweza kumaanisha mambo mengi; inaweza kumaanisha tunda la Roho, ambalo ni upendo, furaha, upole, fadhili; lakini pia inaweza kumaanisha matunda ya huduma. Kama tunavyoona katika Agano Jipya, watu wengine kutoka Kupro na Kurene walikwenda Antiokia, na mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, na umati wa watu ukamgeukia Bwana (ona Matendo 11:19-26).