UJASIRI KATIKA KUOMBA AHADI ZA MUNGU
Biblia inatuambia kwamba Bwana hana upendeleo. Na kwa sababu haonyeshi upendeleo-kwa sababu ahadi zake hazibadiliki kutoka kizazi hadi kizazi-tunaweza kumuuliza atuonyeshe rehema zile zile ambazo ameonyesha watu wake kupitia historia. Hata Mfalme Manase ambaye alifanya dhambi mbaya kuliko mfalme yeyote kabla yake wakati alipotubu, alirudishwa (ona 2 Mfalme 21:1-18).