ANZA KUCHIMBA LEO!

David Wilkerson (1931-2011)

Mathayo inatuambia Yesu alizungumza kwa mifano: "Yesu aliwaambia watu wote kwa mifano ... ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema: Nitamfungua kinywa changu kwa mifano; Nitayatamka mambo yaliyofichwa tangu mwanzo wa ulimwengu" (Mathayo 13:34-35).

Wakristo wengi leo wanafikiri mifano ina rahisi sana lakini kwa mujibu wa Kristo, kuna ukweli wa siri katika kila mfano aliyoambia. Ukweli huu unawezwa kugunduliwa tu kwa kuutafuta kwa bidii. Waumini wengine wanajitokeza juu ya mifano kwa haraka, wakidhani wanaona somo la wazi, na kuendelea na kile wanachokiona "ukweli wa kina." Wanataka teolojia ambayo imewekwa wazi kwao, inaoelezwa kwa undani.

Yesu alisema mfano juu ya hazina iliokuwa ndani ya shamba: "Ufalme wa mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa katika shamba, ambayo mtu alipoiona akaificha; na kwa furaha juu yake akaenda na kuuza alivyo navyo na kununua shamba hilo" (Mathayo 13:44).

Shamba inaashiria eneo lolote ulimwenguni ambapo injili imehubiriwa na kupokelewa. Na mtu anayefanya kazi katika shamba anawakilisha kila mtu anayemtumikia Yesu. Mtu huyu amejifunza kutokana na chanzo cha kuaminika kuwa hazina ni kuzikwa mahali fulani katika shamba - hazina ya kujua kwamba Kristo ni yote anayohitaji. Furaha yote, mwongozo na kusudi, kwa kweli, utajiri wa mbinguni, ni wake ndani ya Yesu. Hivyo wakati wafanyakazi wengine wanafanya kazi kwa shingoupande, yeye huanza kuchimba kwa bidi akijaribu kutafuta hazina.

Kwa mushangawo mkubwa, anapopata hazina, anaificha mara moja. Kwa nini? Kwa sababu anataka kuwa na hakika kwamba haiibiwe. Hataki mtu yeyote au kitu chochote kumzubaza mbali ya ukweli mkubwa aliopata katika Kristo.

Wakati Yesu anasema kwamba mfanyakazi wa shamba "anauza kila kitu anacho na kununua shamba hilo," inamanisha kwetu sisi kubadili utegemeyaji wetu kwa kazi nzuri, hofu yetu na shaka, kwa zawadi yake ya uzima. Tunatumia wakati wetu, mawazo yetu, mapenzi yetu, mipango yetu, kununua maji yaliyo hai, mkate wa maisha, furaha na amani.

Je! Hazina hii ina thamani gani kwako? Ili kumpata, nawahimiza kuanza kuchimba leo!