DAKIKA KUMI NA TANO KILA SIKU

Gary Wilkerson

"Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu maharli palipobomoka, kwa ajili ya nchi" (Ezekieli 22:30).

Mungu anasema anaangalia mtu ambaye ni tayari "kusimama katika pengo," mahali pana, utupu na kitu ambacho hakipo. Uinjilisti, ibada, kufundisha, kuhubiri, kazi njema, shule ya Jumapili, na huduma ya vijana hufunikwa vizuri, lakini "pengo" la kanisa lako linaweza kuwa sala.

Bwana anaita kanisa lake kusimama katika pengo, bila kujali ni matokeo gani. Ikiwa unasali tu kupata mafanikio katika maisha yako mwenyewe, wewe ni kama Mafarisayo - na Yesu akawaita wanafiki au wanaojifanya. Unaweza kujifanya kama mumesimama katika pengo kwa mtu mwingine lakini kwa kweli unataka icho kitu mwenyewe. Ikiwa hutapata kile unachotaka kutoka kwa Mungu, baada ya dakika kumi na tano, unaacha kuomba. Mkutano wa maombi na kutafuta uso wake sio sehemu ya maisha yako - na una shaka kuwa Mungu atajibu sala.

Mungu anataka sala inayoendelea, yauminifu na ya moyo. Kusimama katika pengo mahali pa siri na Mungu kwa dakika kumi na tano kila siku ni mwanzo mzuri. Utapata dakika hiyo kumi na tano kurejea kwa ishirini na kisha thelathini. Usiwe na wasiwasi juu ya muda gani unapoomba, endelea kukaa thabiti.

Biblia inatuambia wazi kwamba anataka tujazwe na upendo na nguvu zake - na hii hutokea tu wakati tunapoingia mahali pa siri pamoja naye. Ikiwa unafanya kazi njema tu ili kuonekana kwa watu, hivi ndivyo utakavyoona maisha yako yakitokomezwa na maswali haya: "Je, waliniona? Je! Wanafurahia kile nimefanya? Je, ninakubaliwa? Je, ninawapenda?"

Unaposimama katika pengo na kumtumikia, haitajali nini wengine wanasema na hutaangalia hilo kofi la nyuma. Macho ya Baba ni juu yako na anasema, "Umefanya vizuri, mtumishi mwema na mwaminifu."