KUHANI MKUU WA AMANI

David Wilkerson (1931-2011)

Yesu alikufa msalabani ili kuninunulia amani na Mungu, na yuko mbinguni sasa ili kudumisha amani hiyo kwa ajili yangu na ndani yangu. Amani tuliyo nayo na Mungu kupitia Kristo inatofautisha imani yetu na dini nyingine zote.

Katika kila dini nyingine kando na Ukristo, swali la dhambi halitatuliwi kamwe. Utawala wa dhambi haujavunjwa. Kwa hiyo, “‘Hakuna amani,’ asema Yehova, ‘kwa waovu.” (Isaya 48:22) , lakini tuna Mungu ambaye hutoa amani kwa kusamehe dhambi. Hii ndiyo sababu hasa iliyomfanya Yesu aje duniani: kuleta amani kwa wanadamu wenye matatizo na woga. Yesu anadumishaje amani ya Mungu kwa ajili yangu? Anafanya kwa njia tatu.

Kwanza, damu ya Kristo iliondoa hatia ya dhambi yangu. Kwa maana hii, Paulo anasema, “Kwa maana yeye ndiye amani yetu” (Waefeso 2:14). Yesu alifanya amani kwa ajili yangu kwa damu yake.

Pili, Kristo hudumisha amani na furaha yangu katika imani. “Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu” (Warumi 15:13).

Tatu, Yesu ananifanya nishangilie kwa tumaini la kuingia katika utukufu. “Tunafurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu” (Warumi 5:2).

Kwa ufupi, amani ni kutokuwa na woga, hivyo maisha bila woga ni maisha yenye amani. Yesu alipopaa mbinguni, hakufurahia tu utukufu ambao Mungu alimpa. Hapana, alikwenda kwa Baba ili kudumisha amani iliyopatikana kwa bidii ambayo alitupatia pale Kalvari.

Mwokozi wetu yu hai katika utukufu sasa hivi, na yeye ni Mungu kamili na mwanadamu kamili mwenye mikono, miguu, macho na nywele. Pia ana makovu ya misumari kwenye mikono na miguu yake pamoja na jeraha ubavuni mwake. Hajawahi kuutupilia mbali ubinadamu wake; bado ni mtu katika utukufu. Hivi sasa, mtu wetu katika umilele anafanya kazi ili kuhakikisha kuwa hatuibiwi kamwe amani aliyotupa wakati anaondoka. Anahudumu kama kuhani wetu mkuu, akishiriki kikamilifu katika kuweka mwili wake duniani ukiwa umejaa amani yake. Na anapokuja tena anataka “tupatikane naye katika amani” (2 Petro 3:14).