JE! NINI KINATOKEA WAKATI KUTOKUAMINI KUNAWEKWA NDANI?

David Wilkerson (1931-2011)

"Msifanye mioyo yenu kuwa mingumu kama wakatika wa kukasirisha, siku ya kujaribiwa jangwani, ambapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, na wakona matendo yangu yangu miaka arobaini. Kwa hiyo nilichukizwaa na kizazi hiki, nikasema, "Daima hupotea moyoni mwao, wala hawakuzijua njia zangu." Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, "Hawataingia katika raha yangu" (Waebrania 3:8-11).

Ni sababu gani inayotolewa kwa nini watu wa Mungu hawakuweza kuingia katika mapumziko yake? Je, ni kwa sababu ya uzinzi, tamaa, ulevi? La, ni kwa sababu ya kutokuamini pekee. Hapa kulikuwa taifa lililo wazi kwa miaka arbaini ya miujiza, miujiza isiyo ya kawaida ambayo Mungu alifanya kazi kwa niaba yao. Kwa kweli, hakuna watu wengine duniani walipendwa sana, na kwa kuwajali sana kama hivo.

Walipokea ufunuo baada ya ufunuo juu ya wema wa Bwana. Waliposikia neno safi lililohubiriwa mara kwa mara na Musa, kiongozi wao na nabii wao, na bado, hawakuchanganya neno hilo pamoja na imani. Kwa hiyo, kusikia hakukuwafanya vizuri. Katikati ya baraka hizo zote, bado hawakuamini Mungu kuwa mwaminifu, na baada ya muda, kutokuamini kuliwekwa ndani yao.

Wapenzi, ukosefu wa imani ni sababu ya msingi wa ugumu wa moyo wote. Andiko linaendelea, "Tena ni akina nani aliochukizwa nao miaka arobaini? Si wale waliokosa. Ambao mizoga yao ilianguka katika jangwa?" (Waebrania 3:17). Kutoamini kwa watu uliweka ghadhabu ya Mungu dhidi yao; Zaidi ya hayo, ikawafanya kuwa wagumu kwa kudumu kwa kutokuamini: "Jihadharini, ndugu, pasiwe katika mmoja wenu ana moyo mbovu wa kutokuamini kwa kujitenga na Mungu aliye hai ... ili mmoja wenu asifanywe mugumu kwa udanganyifu wa dhambi" (3:12-13).

Kutokuamini pia ni mzizi wa uchungu wote, uasi na ubaridi. Ndio maana Waebrania sura ya 3 huelekezwa kwa waumini. Unaweza kuokolewa, kujazwa Roho, na kutembea kwa utakatifu mbele ya Mungu na bado una hatia ya kutokuamini. Ni muhimu sana kukubali nguvu zake zisizo za kawaida kwa imani na kusema kwa ujasiri, "Fanya tena, Bwana. Na nguvu zako ziwe kamili katika udhaifu wangu."