KAMA VILE YESU MWENYEWE ALIKUWA AKIOMBA

David Wilkerson (1931-2011)

Kudai nguvu katika jina la Kristo sio ngumu, ukweli ya mambo aliofichwa ya kitheolojia. Nyumba zinazohifazi vitabu vyakusoma tu juu ya suala la jina la Yesu ambalo waandishi waliandika kusaidia waumini kuelewa maana ya kina kiliyofichwa kwa jina la Kristo. Hata hivyo, wengi wa vitabu hivi ni "kina," huenda juu ya vichwa vya wasomaji.

Ninaamini ukweli kwa kile tunachotakiwa kuelewa kuhusu jina la Yesu ni rahisi sana kwamba mtoto anaweza kuielewa. Ni jambo hili tu: tunapofanya maombi yetu kwa jina la Yesu, tunapaswa kuwa na uhakika kabisa kwamba ni sawa na kwamba Yesu mwenyewe alikuwa akiomba Baba. Inawezekanaje kuwa  ukweli?

Tunajua kwamba Mungu alimpenda Mwana wake. Alizungumza na Yesu na kumfundisha wakati wake duniani, na Mungu si hakusikia tu ombi lolote liliofanywa na Mwanawe lakini aliyajibu. Kwa kifupi, Baba hakukanusha ombi lolote kutoka kwa Mwanawe.

Leo, wote wanaomwamini Yesu wamevaa Uzazi Wake. Na Baba wa mbinguni hutupokea kwa uangalifu kama anavyopokea Mwana wake mwenyewe. Kwa nini? Ni kwa sababu ya umoja wetu wa kiroho na Kristo. Kupitia kusulubiwa na kufufuka kwake, Yesu ametufanya kuwa mmoja na Baba. "Ili wote wawe na umoja; kama Wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, na mimi ndani yako; hao nao wawe ndani yetu ... Mimi ndani yao, na Wewe ndani yangu" (Yohana 17:21 na 23).

Kwa kueka kama kawaida, sisi sasa ni familia - mmoja na Baba, na mmoja na Mwana. Tumekubaliwa, na haki kamili za urithi ulio na mtoto yeyote. Hii ina maana nguvu zote na rasilimali za mbinguni zinapatikana kwetu - kupitia Kristo. Na kwa sababu tumevaa katika Uzazi wa Kristo, tunajua maombi yetu pia yanasikia na Baba. Anajibu maombi yetu, kama vile alivyojibu yale ya Mwanawe.

Ni mamlaka ya ajabu ambayo tumepewa wakati tunapoomba kwa jina la Yesu.