KUTOJIFANYA KUWA MWENYE SIFA

Gary Wilkerson

Yesu alikuwa na moyo wa mtumishi na anatuita kufanya utumishi. "Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayonilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; amabaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba" (Wafilipi 2:5-8).

Ninataka kukupa mambo sita ambayo Yesu anataka kutuambia leo kuhusu kutumikia:

  • Mtumishi mwenye kutojali kuhusu sifa yake.
  • Kama mtumishi, tunajali zaidi juu ya yale Mungu anayofikiria kwetu kuliko kile ambacho wengine wanachofikiria.
  • Mtumishi asiye kuwa barafu kwa mashaka yake mweyewe au kusema mengi zaidi.
  • Mtumishi anatumika kulingana na mipango na makusudi ya Mungu, kwa uongozi wa Roho Mtakatifu.
  • Mtumishi hufanya huduma zake bila hisia ya kiburi.
  • Mtumishi wa kweli hutumika kama Yesu alivyofanya - na ulimwengu unaona tofauti.

Utumishi wa kweli unajitoa, ni unyenyekevu, na hutafuta mema ya wengine - kuheshimu wengine zaidi kuliko tunavyojiheshimu. Hatuwezi kujisikia kila wakati kama kutumikia, bila shaka. Tunaweza kutumikia vizuri wakati mambo yanaendelea vizuri lakini hali mbaya huwa inapunguza nguvu zetu kwa kuwafikia wengine.

Kwa mujibu wa hatua ya kwanza hapo juu, Yesu "hakujifanya kuwa mwenye sifa." Tabia yetu inapaswa kufanana na hiyo ya Yesu, ambaye hakufanya mambo kutokana na tamaa ya ubinafsi au haja ya kutambuliwa. Aliweka hali yake mwenyewe na kufariji kuwa kando ili afanye kazi kwa wema wa wale walio karibu naye.

Je, maisha yako hufanya tofauti ambazo dunia inachukua kama mfano? Mshahara, utambuzi wa umma au shukrani haipaswi kuwa motisha yetu ya kuishi inje ya utumishi wa kweli kama Yesu alivyofanya. Lakini ni furaha gani huleta Mwokozi wetu tunapofuata katika nyayo zake - na hiyo ndiyo malipo yetu ya kweli.