KWA NINI YONA ALIKIMBIA?

David Wilkerson (1931-2011)

"Basi Neno la Bwana lilimjia Yona ... likisema, 'ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa, ukapige kele juu yake; kwa maana uovu wao umepanda juu mbele yangu "Lakini Yona akaondoka akimbilie Tarshishi" (Yona 1:1-3).

Tunajua hadithi ya Yona, mtu ambaye alijaribu kukimbia kutoka kwa Mungu wakati Bwana alimpa mamlaka ya kuhubiri hukumu kwa mji wa Ninawi. Lakini badala ya kuonya Nineve, Yona alikimbia. Hadithi hii ilithibitishwa na Kristo mwenyewe: "Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa arthi" (Mathayo 12:40) . Kwa maneno mengine, hadithi ya Yona ilikuwa na hakika kama mazishi ya Kristo mwenyewe na ufufuo wake.

Kwa nini Yona alikataa kutii Neno la Mungu lililo wazi wazi na kukimbia? Kwa wazi Yona alikuwa na vipawa na alichaguliwa na Mungu, lakini yeye alikimbia mbele ya Mungu sana, akiwaachilia ushirika pamoja naye. Yona alipokimbia, alisikia sauti ya Roho Mtakatifu akizungumzia masikioni mwake kwa kila hatua alio piga.

Yona alipewa ufunuo wenye nguvu wa neema na huruma ya Mungu: "Najua ya kuwa Wewe ni Mungu mwenye rehema na mwenye huruma, si mwepesi wa wa hasira, u mwingi wa rehema" (4:2). Bila shaka, Mungu ni kila kitu ambacho Yona anaelezea lakini Biblia pia inazungumzia juu ya utakatifu wa Mungu, hali ya haki. "Kwa maana ghadhabu ya Mungu Imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu" (Warumi 1:18).

Ninaamini Yona hakumtii kwa sababu alidhani, "Bwana, kila wakati utakaposema hukumu, wewe unazidiwa na huruma. Najua huwezi kuhukumu Ninawi kwa sababu mara tu nitakapotaounabi, watatubu na utawafufulia neema yako juu yao. "Yeye hakuwa na ufahamu wa hofu ya Mungu, wutakatifu wake, mwenye haki.

Kila mwamini lazima ashikilie ufunuo wa hofu ya Mungu kama ilivyofunuliwa katika Neno lake: "Mche Bwana Ukajiepushe na uovu" (Methali 3:7). Kama rehema ya Mungu, hofu ya Mungu ni kutoa maisha - "Kumcha Bwana ni chemchemu ya uzima" (14:26) - na tunapaswa kujifunza kusawazisha ma wili hayo.