TUNASHAUKU KUBWA KWA AJILI YA KUNGOJEA KURUDI KWAYESU

David Wilkerson (1931-2011)

Yesu anakuja hivi karibuni! "Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni kwa kupiga kelele, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu. Nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai na tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumulaki Bwana angani. Na kwa hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Kwa hivyo farijianeni mioyo yenu kwa maneno haya” (1 Wathesalonike 4:16-18).

Kwa Kiebrania, neno "kupiga kelele" linamaanisha kuchochea kwa neno, kuamsha, kusikika kwa matendo. Washindi wote watasikia sauti ya malaika mkuu: "Yuko mlangoni! Yeye unayempenda amekuja kuchukua wewe!” Huo sio kuja kwa kimya kimya, kufanywa kimya kimya kwenye kona. Hapana! Yesu anakuja na barapanda ya baragumu, na majeshi ya malaika, na kelele, na sauti kubwa ya mbinguni ya malaika mkuu. Wafu katika Kristo watafufuka kwanza kukutana naye angani na hiyo itakuwa shangwe ya ngurumo gani. Kisha atatuma malaika wake katika ulimwengu wote na kukusanya watoto wake kwake.

Katika historia yote, tofauti zimetabiriwa kwa upumbavu wakati wa kurudi kwa Kristo. Maelufu ya watu wengi wameuza yote waliyonayo na wamekwenda kwenye mahari maalum kungojea kurudi kwake - lakini wamekosa. “Angalieni,  na mkeshe kwa kuomba; kwa maana hamjui wakati utakapokuwapo” (Marko 13:33). Jihadharini na kucukuliwa wakati gani na jinsi gani Yesu anakuja, wakati unapaswa kuzingatia ni nani anaokuja. Mungu amezuia wakati wa kurudi kwa Kristo kwa ajili ya kuweka watu wake katika hali ya kukesha.

"Yesu huyu, ambaye anachukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo kama vile mulivyomuona akienda mbinguni" (Matendo 1:11). Ni Mtu aliyetukuzwa aliyeondoka na ni Mtu anayetukuzwa ambaye anarudi! Je! Ungetamani kuwa na Bwana? Je! Ulijua kwamba ni hamu yake ya kuwa na wewe? Kuishi kila siku kwa kutarajia kwa furaha kuja kwake saa yoyote. Na kumbuka kuwa mpaka atakapokuja, kuna kazi nyingi inayopaswa kufanyika!