WAKATI MUNGU ANATUITA KUTENDA

David Wilkerson (1931-2011)

Umesikia juu ya sala ya imani lakini naamini kuna picha ya kioo ya sala hii inayotokana na mwili - sala ya kutokuamini. Sala kama hiyo haikubaliki kabisa kwa Mungu; Kwa kweli, Maandiko inasema ni dhambi machoni pake.

Musa, mtu wa Mungu, mwenye kuomba ambaye alikuwa amewufuata wito wa Mungu kwa kila hatua alikuwa anapiga ikaja kwenye mgogoro katika maisha yake. Waisraeli walikuwa wakifukuzwa na Mfalme Farao na hapakuwa na matumaini kabisa ya kukimbia isipokuwa kupitia Bahari ya Shamu. Musa alijua moyoni mwake kwamba mgogoro huu uliwekwa na Mungu na bado, kilio cha hofu cha mamia ya maelfu ya watu kilikuwa kikilia masikioni mwake, kwa hiyo akaenda kwenye mlima wa upeke na kumwaga moyo wake kwa maombi makubwa. Mungu hakuchika kwa upole kuhusu usiku wake wote wakulia kwa sababu ilikuwa ni ushahidi wa mzizi wa kutoamini katika moyo wake.

Ninasema kwamba umewahi kusikia Bwana akikuambia, "Acha kulia na inuka kutoka kwa magoti yako." Lakini Bwana akamkemea Musa, "Mbona unanililia mimi?" (Kutoka 14:15). Maana halisi ya Kiebrania kwa mstari huu ni, "Mbona unaniungulumia?"

Kwa nini Mungu alisema hii kwa Musa? Kwa sababu Mungu alipomwita Musa kuwaokoa wana Israeli, aliahidi kumpa sauti ambayo watu wangeisikiliza (angalia Kutoka 3:18). Hata hivyo, Musa alijibu kwa kutokuamini, "Lakini, tazama hawataamini wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, 'Bwana hakukutoke'" (4:1).

Fikiria jinsi upumbavu wa kutokuamini kwa Musa ulikuwa. Kwa nguvu za Mungu, alikuwa tayari amefanya maajabu makubwa na baadaye alipata ushirika wa karibu na Mungu. Lakini hapa katika Bahari Nyekundu, alisisitiza kwa kuwa na shaka ya kutokuamini, na Mungu aliamuru, "Chukua mamlaka ya kiroho juu ya mgogoro huu na kuendelea mbele katika imani. Masaa kutoka sasa, utakuwa ukicheza kwa furaha."

Tunapopatwa na matatizo yetu wenyewe, tunaweza kujiamini kuwa sala ni jambo muhimu zaidi tunaweza kufanya. Lakini wakati unakuja wakati Mungu anatuita sisi kutenda, kutii Neno lake kwa imani, ili sala zetu zisipatikane kwa kutokuamini.