ZAWADI KUTOKA KWA MUOKOZI

Nicky Cruz

"Nami nitamwomba Baba naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele – ndiye Roho wa kweli  ... Bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakua ndani ndani yenu" (Yohana 14:16-17).

Mungu ndiye mtoaji wa zawadi za kushangaza, na za ajabu. Lakini kuna jambo kama vile kutojua jinsi ya kupokea. Hilo lilikuwa jambo kwangu wakati mtoto wangu wa kwanza, Alicia, alipofika. Nilikuwa bado nijaribu kujua jinsi ya kuwa mume mzuri kwa bibi yangu mzuri, Gloria, na ghafla nimejikuta nikabiliana na kazi ya kuwa baba kwa msichana mdogo.

Miaka michache iliyopita mwanasaikolojia aliyechaguliwa na mahakama aliniambia kuwa sitakuwa tena mtu wa kawaida kwa sababu ya maisha yangu ya zamani yenye kutisha. Pia aliniambia, "Una upande wa giza ... na hujui jinsi ya kupenda au kupendwa." Maneno hayo yalinikosesha amani.

Tangu wakati huo tulileta nyumbani Alicia kutoka hospitali, Gloria angeweza kusema kitu kibaya katika majibu yangu kuhusu yeye. Ningepiga magoti juu ya kikapu cha binti yetu na kusugua uso wake kwa mikono yangu lakini sikuwahi kumunyanyuwa. Alicia alipokuwa na wiki nne, Gloria aliniuliza kwa nini sikutaka kumtunza mtoto, na nilimwambia, "Sijui jinsi gani." "Basi acha nikuonyeshe," alisema.

Kama nilivyomtunza binti yangu na kujisikia huruma kubwa na upendo unaoendesha kupitia moyoni mwangu, kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilielewa nini maana ya kuwa baba. Na pia katika wakati huo, hatimaye nilielewa maana ya kupokea zawadi isiyoweza kutenganishwa kutoka kwa Mwokozi.

Kama mwamini katika Bwana Yesu Kristo, umepewa kipawa kisichoweza kulinganishwa na Mungu - zawadi ya Roho Mtakatifu. Mungu amewapa kila mmoja wa wafuasi wake kiwango cha nguvu zake, kipande kidogo cha yeye mwenyewe. Ni zawadi ambayo hakuna hata mmoja wetu anayestahili, na moja ambayo hatuwezi kulipa tena, hata hivyo hutoa kwa uhuru na kwa hiari kwa wote wanaoweka imani yao kwake. Zawadi hii haipaswi kuchukuliwa vyema na anataka ujifunze kuipokea kikamilifu.

Nicky Cruz, mwinjilisti wa kimataifa aliyejulikana na mwandishi mkubwa, alimgeukia Yesu Kristo kutoka kwenye maisha ya vurugu na uhalifu baada ya kukutana na David Wilkerson huko New York City mwaka 1958. Hadithi yenye kushangaza  ya kuokoka kwake ilisemwa mara ya kwanza katika Musaraba na Kisu kinachomoka ( Cross and Switchblade) na David Wilkerson na kisha baadaye katika kitabu chake chenye kuuzwa vizuri zaidi, kiitwaco:Kimbiya , Mtoto, Kimbiya (Run, Baby, Run).