KUMPA MUNGU KILA KITU TULICHO NACHO
“Kwa hiyo Bwana atangojea, ili apate kuwa mwenye neema nanyi; na kwa hivyo atainuliwa, ili apate kuwahurumia. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki; wamebarikiwa wote wamngojeao. Kwa maana watu watakaa katika Sayuni huko Yerusalemu; hutalia tena. Atakuwa mwenye neema sana kwako wakati wa kilio chako; akiisikia, atakujibu” (Isaya 30:18-19). Isaya alikuwa akisema, "Ikiwa utamngojea Bwana, ikiwa utamlilia tena, na kurudi kumwamini-atakufanyia kila kitu nilichosema na zaidi."