KUHIFADHIWA KUTOKA KWA KUUANGUKIA NJE
Katika barua kwa Wakristo wa Thesalonike, Paulo anasema juu ya tukio la siku zijazo anaiita "siku ya Bwana." Anaandika, "Basi, ndugu, tunawasihi, kwa habari yakuja kwake Bwana Yesu Kristo na kukusanyika kwetu mbele zake, msikatishwe tamaa au kushitushwa na mafundisho yanayodaiwa kutoka kwetu - iwe ni kwa unabii au kwa kinywa; au kwa barua ikidai kwamba siku ya Bwana tayari imefika. Msiruhusu mtu yeyote awadanganye kwa njia yoyote, kwa maana siku hiyo haitakuja mpaka uasi utokee, na mtu wa uasi afunuliwe” (2 Wathesalonike 2:1-3, NIV).