KUFUNIKWA NA DAMU YA KRISTO
Hakuna mtu anayeweza kuhesabu rehema nyororo zote za Kristo na baraka nyingi za damu yake iliyomwagika. Lakini wacha tuangalie ushindi mmoja haswa: msamaha wa dhambi zote za zamani.
"Tukitembea katika nuru kama yeye alivyo nuruni, tuna ushirika sisi kwa sisi, na damu ya Yesu Kristo Mwanawe hututakasa na dhambi zote… Tukikiri dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki kutusamehe dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote” (1 Yohana 1:7, 9).