Hivi majuzi, nilimwendea Bwana katika maombi nikiwa na huzuni sana, nikiwa nimeelemewa na mahangaiko mengi. Nilianza kusihi kesi yangu mbele yake, “Ee, Bwana, sijawahi kuchoka sana katika maisha yangu yote. siwezi kuendelea.” Niliishiwa nguvu sana machozi yalinitoka. Nikiwa nimelala huku nikilia, niliwaza, “Hakika machozi yangu yatausukuma moyo wa Bwana.”
Roho Mtakatifu kweli alikuja na kunihudumia, lakini si kwa jinsi nilivyofikiri angefanya. Nilitaka huruma, kutiwa moyo, kuelewa; na alinipa yote hayo lakini kwa njia tofauti sana na nilivyotarajia.