Body

Swahili Devotionals

KUSHIKAMANA NA YESU KWA MOYO WAKO WOTE

Gary Wilkerson

"Basi petro na Yohana walikuwa wakienda pamoja kwanda hekaluni, saa ya kuomba, saa tisa. Na mtu mmoja alieyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye ... ili aombe sadaka ... Lakini Petro akasema, "Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, Simama uende ... na mara moja [miguu ya mtu] na nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu. Na akainuka upesi, akasimama na kuanza kutembea" (Matendo 3:1-2, 6-8).

JE! TUMEWASAHAU WALE WALIOFUKUZWA?

Nicky Cruz

Je! Tunajitleaje kuhusu watu waliotengwa na jamii yetu? Je, utamaduni wetu unafanya nini kwa maskini, watumiaji wa madawa ya kulewa, walevi, wanachama wa genge, mashoga, wagonjwa wa UKIMWI, wenye dhambi? Muhimu zaidi, Mwili wa Kristo unafanya nini nao? Je! Tunawaona kama watu wanaohitaji msaada, waliopotea na kutafuta njia ya kutovunjika moyo na utumwa? Au Je! tunajifanya kama hawako? Je! Tunawazuia bila kuona, mahali fulani mbali na macho yetu, kwa hivyo hatupaswi kukabiliana nao?

VITA YA KUKUMBUKA WEMA WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Asafu, mtunga-Zaburi aliyeandika Zaburi ya 73, alikuwa rafiki wa karibu wa Mfalme Daudi. Mtu mwenye moyo safi aliyeamini katika wema wa Mungu, alianza hotuba yake katika Zaburi hii kwa kusema, "Hakika Mungu ni mwema kwa Israel, kwa kweli hao walio na mioyo safi" (73:1). Kwa maneno mengine, "Mungu amekuwa mzuri kwangu kwa kunipa moyo safi." Lakini katika aya inayofuata, mtu huyu mpendwa anakiri, "Nilipoteza! Nili karibia kuanguka katika dhambi. "Kwa nini Asafu anasema jambo hili?

ALICHAGUA KUWA BABA YAKO

David Wilkerson (1931-2011)

Wakristo wengine kwa kweli hushindwa na hofu. Baadhi daima huwa na wasiwasi wakati wengine wanapokuwa na hatia, wakiogopa hawaweza kushinda dhambi kamwe. Wanaogopa kupoteza kazi zao, afya zao, familia zao. Hawana kabisa amani, furaha au kupumzika. Hiyo ni wakati ninasikia Yesu akiuliza, "Je, nimekuwa nanyi muda mrefu na bado hamjaona? Je, hujui Mungu kama Baba yako?"

Kutokana na urafiki wa karibu na Kristo lazima kuja ufunuo kwamba una Baba mbinguni ambaye ameonyesha wazi jinsi alivyo na nini anatamani kuwa kwako!

NINI KINACHOSUKUMIA YESU KUTENDA

David Wilkerson (1931-2011)

Wakristo wengi wanaoishi leo wanapenda kufikiri kwamba, kama Yesu, "wanasukumwa pamoja na huruma." Wakati alikuwa  hapa dunia, Yesu alikuwa mfano wa huruma  kutoka kwa Mungu. Maandiko mara nyingi husema kwamba Kristo alikuwa "mwenye huruma" kwa mateso ya watu. Na ikiwa ndivyo ilivyokuwa katika karne ya kwanza, ni lazima huzuni kubwa kuna nini sasa katika moyo wa Bwana.

Biblia inatuambia, "huruma Zake hazipunguki" (Maombolezo 3:22). "Lakini wewe, Bwana, U Mungu wa rehema na neema, Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli" (Zaburi 86:15).

BABA AMEFUNULIWA

David Wilkerson (1931-2011)

Katika Agano la Kale, watoto wa Mungu walikuwa na picha tu ya Mungu kama Baba yao. Daudi alisema, "Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao" (Zaburi 103:13). Isaya alimwita Mungu "Baba wa milele" (Isaya 9: 6), na Yeremia aliandika juu yake, "Utaniita mimi, 'Baba yangu'" (Yeremia 3:19).

KWA SABABU MTU ASIYE NA KITU ALIKUTANA NA YESU

Gary Wilkerson

"Maana, ndugu zangu angalieni mwito wenu, yakwamba si wengi wenye hekima ya mwili, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa ... Bali Mungu aliachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima ... vitu ambavyo haviko, ili avibadilishe vile vilivyoko; mwenye wmili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu. Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu ... kusudi, kama ilivyoandikwa, "Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana" (1 Wakorintho 1:26-31).

MUNGU HAJAWAHI KUSHINDISHA WATU WAKE

Carter Conlon

Kwa mujibu wa kitabu cha Waebrania, kila mmoja wetu anapaswa "Lakini zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu" (Waebrania 10:32). Kumbuka jinsi Mungu mwaminifu amekuwa - jinsi alivyokulete kupitia mapigano na majaribio yako yote ya zamani. Wakati ulipofika kwa Kristo kwanza, labda familia yako yote ilidhani wewe ni wazimu; marafiki wako wa zamani hawakutaka kuwa na wewe tena. Watu wanakuhukumu mahali pa kazi kwa sababu tu ulichagua kufanya yaliyo sawa. Na sasa, tena, unakabiliwa na mashtaka mabaya kutoka pande zote.

KUTAFUTA MAPUMZIKO KWA NAFSI ILIYOOGOPA

David Wilkerson (1931-2011)

Yesu alikuja duniani kama mtu wa kuwakomboa wanadamu kutoka kwa dhambi zetu na kila aina ya utumwa. Lakini pia alikuja duniani kwa lengo la kutufunulia Baba wa mbinguni.

Aliwaambia wanafunzi wake, "Baba amenituma" (Yohana 5:36). Pia alisema, "Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe ... Siyatafuti mapenzi Yangu mimi, bali mapenzi ya Baba aliyenituma" (Yohana 5:30). Kisha akasema, "Naenda kwa Baba Yangu" (Yohana 14:12).

UKOSEFU WANGU WA HURUMA

David Wilkerson (1931-2011)

Yesu alisema mfano kuhusu mtumishi ambaye alisamehewa deni kubwa. Mtu huyu alipata fadhili na huruma kwa bwana wake, lakini alichukua yote kwa nafasi. Mara baada ya kusamehewa, akaondoka na kuanza kumchochea mtu ambaye alipaswa kulipa deni lake kidogo, akisema, "Nipe deni langu - sasa!" Wakati mdaiwa alimwomba yule msamaha, alikataa na mdaiwa alifungwa.