Body

Swahili Devotionals

JIFANANISHE NA KRISTO PEKEE

David Wilkerson (1931-2011)

Moyo wa ujumbe wa kweli wa neema sio injili ya vibali lakini moja ambayo hufundisha utakatifu!

"Kwa maana neema ya Mungu iwaokayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa katika ulimwengu huu wa sasa; tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu." (Tito 2:11-13).

KUKUBALIWA NA BABA

David Wilkerson (1931-2011)

"Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu"  (2 Wakorintho 5:21).

Ninaamini kuwa haki kwa imani ni ukweli wa msingi wa Ukristo. Huwezi kujua mapumziko ya kweli na amani hadi ufikiri kwamba huwezi kamwe kuwa sahihi machoni pa Mungu kwa kazi zako mwenyewe.

KUTEMBEA KATIKA AHADI ZA MUNGU

Gary Wilkerson

Wakati Yoshua alipopewa ma muraka ya kuwa kiongozi wa taifa la Waisraeli, Mungu alisema kwa maneno mazito kuhusu yeye . "Je! Si mimi niriye kuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendapo" (Yoshua 1:9).

MUNGU HUJA KUPITIA KATIKATI YA MACHAFUKO

David Wilkerson (1931-2011)

Daudi alikuwa mtu mwenye imani kubwa ambaye aliekua kiumungu, mwenye hekima, mufalme mpendwa. "Naye Daudi akafanikiwa katika kazi zake zote, kwa kuwa Bwana alikuwa pamoja naye" (1 Samweli 18:14, ESV). Alikuwa mtu wa sala nyingi, akimsifu Bwana, kama watu wachache waliowahi kufanya, na kubariki moyo wa Mungu kwa nyimbo zake. Hakuna mtu aliyeweza kuwa karibu sana na Bwana kuliko Daudi.

MTU WA IMANI

David Wilkerson (1931-2011)

Abrahamu anajulikana kwa kanisa kama mtu wa imani. Hakika, Biblia inamtumikia kama mfano wa imani: "Kama vile Ibrahim alivyo mwamini Mungu akahesabiwa haki" (Wagalatia 3:6).

Mungu alikuwa amemtokea Abramu (kama alivyoitwa hapo) na akasema, "Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana! "(Mwanzo 15:1). Mungu pia aliahidi Abramu kwamba angezikwa "uzee mwema" (angalia mstari wa 15). Na kuna zaidi! Zaidi ya hayo, Mungu aliahidi kwamba mtu yeyote aliyejaribu kumdhuru au kumlaani Abramu mwenyewe angelaaniwa (angalia Mwanzo 12:3).

FAIDA ZA TOBA

David Wilkerson (1931-2011)

Tunamjua Danieli kama kijana mwenye nguvu, aliyepewa vipawa ambaye alimtumikia Nebukadneza, mfalme wa Babubuloni kwa uaminifu, na kutafsiri ndoto zake. Lakini matumizi yake makubwa yalikuwa kama matokeo ya kuwa mtu mwema wa sala.

Danieli aliishi maisha ya kujitolea, ya utakatifu ambayo hutaraji kumpata kutubu mbele ya Bwana. Lakini moyo wake ulikuwa anaguswa sana na dhambi na aligundua kwa pamoja dhambi za kutisha za watu wa Israeli. Angalia matumizi yake kwa neno la wingi sisi katika sala yake.

MOYO ULIO WAZI KWA MWANGA HALISI WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Naamini toba ni sawa kwa waumini kama ni kama vile kwa wenye dhambi; Wakristo ambao huendelea kuwa na hisia ya kutubu, inawaletea juu yao tahadhari maalum ya Mungu. Ikiwa tunatembea mbele ya Bwana kwa moyo wenye kutubu, tutafurahishwa na baraka za ajabu.

Tabia inayojulikana ya moyo unaotubu ni nia ya kukubali lawama kwa kwakutenda mauovu, ukisema, "Bwana, mimi ndiye nilietenda dhambi."

MUNGU HANA TATIZO KUKUPATA WEWE

Gary Wilkerson

Haijali jinsi giza linakuzunguk au "haujulikani" utambulisho wako, wakati Mungu anachagua kujidhihirisha kwako mwenyewe, hana shida kukupata wewe. Hebu tuangalie mama wa Samson ... mtu mwenye nguvu aliyewahi kuishi.

"Wana wa Israeli wakafanya tena yaliyo mabaya mbele za macho ya BWANA, BWANA akawatia katika mikono ya wafilisti muda wa miaka arobaini. Palikuwa na mtu mmoja wa Sora ... jina lake akiitwa Manoa; na mkewe alikuwa tasa, na hakuzaa watoto. Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke akamwambia, 'Tazama … nawe utamzaa mtoto mwanamume'" Waamuzi 13:1-3).

AHADI YA YESU KWA AJILI YA UTOAJI WA KILA SIKU

Carter Conlon

Yesu mwenyewe alisisitiza umuhimu wa Neno wakati alitupa namna maalum ya kuomba: "Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, mapenzi yako atimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. Utupe leo mkate wa kila siku" (Mathayo 6:9-11). Juwa kwamba aliielezea kama "mkate wetu wa kila siku." Kuna utoaji wa kila siku ambao Yesu ameahidi kutupa.