Body

Swahili Devotionals

WALIKUWA HURU NDANI YA TANURU!

David Wilkerson (1931-2011)

Sisi sote tunajua hadithi vizuri. Mfalme Nebukadneza, mtawala wa Babloni, aliita kila kiongozi kutoka katika ufalme wake wa mbali ili kukusanyika pamoja ili waheshimu miungu ya uongo. Mfalme alijenga sanamu kubwa, dhahabu na kujaza viongozi wenye kuvaa mavazi ya kuvutia – wakuu wa majimbo, wana wa mfalme, mahakimu na maafisa wa majimbo - pamoja na watu wote wa nchi walipaswa kuzingatia amri ya mfalme na kuinama mbele ya sanamu. Je! Na kama hawangerifanya hivo? Ilikuwa ni hukumu ya papo hapo ya kifo.

UNAKARIBIA KUWA HURU!

David Wilkerson (1931-2011)

Biblia inaonyesha wazi kwamba nguvu za pepo ziko kwenye kazi kwa kuweka mitego kwa Wakristo. Shetani ameamua kabisa kuharibu kila mwamini anayeenda katika utakatifu na kujitolea kamili kwa Yesu Kristo. Sasa elewa, Shetani haupo popote - hawezi kuwa popote mara moja - na hajui mambo yote. Lakini anacho kama amri yake kwa mapepo mengi, mamlaka na nguvu za giza. Na nguvu hizi za giza zinaweka mitego kwa ajili yako. "Watendao uovu wamenitegea mtego" (Zaburi 119:110). "Katika njia niendayo wamenifichia mtego" (Zaburi 142:3).

WAO WANAABUDU BURE

David Wilkerson (1931-2011)

Mungu huchukua suala la ibada kwa umakini sana. Sio kitu cha kuangaza kinakuja katika nyumba ya Mungu, mahali palipobarikiwa na kutiwa mafuta na Roho Mtakatifu. Musa akamwambia Haruni, "Bwana alilolinena, akisema, Nitatakaswa mimi katika hao wanikaribiao, nami nitatukuzwa mbele ya watu hao wote." (Mambo ya Walawi 10:3).

KUCHUNGULIA KWA MAKINI NDANI YA KABURI HALINA KITU

David Wilkerson (1931-2011)

Katika Yohana 20, tunasoma hadithi ya Maria Magdalena, ambaye alisema kwa kifupi Bibi arusi ambaye moyo wake umepewa kabisa Kristo. Inaonekana mwanamke mwenye maana, alihudumia mahitaji ya Yesu kwa upendo na kushikamana akiambatana pamoja na Maria mwingine katika maisha yake. Alifanya hivi kwa shukrani kubwa, kwa maana Biblia inasema kwamba Yesu alikuwa amefukuza pepo saba kutoka kwake (tazama Luka 8:2).

UWEPO WA YESU NDANI YETU

Gary Wilkerson

Agano jipya linasisimua sana - linatuonyesha kwamba Yesu ndiye uwakilishi halisi wa Baba na wakati tunamwona Yesu, tunaona hasa jinsi Mungu alivyo. Ni mwenye kujaa upendo, neema, huruma, nguvu, kweli na haki! Neno la Mungu linatuambia kwamba tumechukua asili yake ya kimungu kwa sababu ya uwepo wa Yesu ndani yetu.

KUWA NA SHAUKU KATIKA UPENDO PAMOJA NA YESU

David Wilkerson (1931-2011)

Ninaamini ibada kuu ya Mkristo inachukuliwa kwenye mistari ya mbele, katika joto la vita, na moto unazunguka pande zote. Kwa kweli, najua waumini wengi ambao ibada yao imeimarishwa katikati ya shughuli nyingi na vita vya kiroho. Hawapaswi kuwa juu ya mlima ili kumpenda kwa moyo wote; hawana haja ya kuishi katika kijiji fulani pekee ili kutamani kuja kwake. Wamejifunza kumpenda Yesu kama mwenye shauku wakati wa kuendesha kwao kwa kufanya kazi kama wakati walipo katika chumba chao chenye sili kwaajili maombi.

YESU ANARUDI

David Wilkerson (1931-2011)

"Kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja" (Mathayo 24:44).

Bibi arusi wa Kristo ni kuishi daima, matumaini ya furaha ya kurudi kwake kwa sababu anaweza kuja wakati wowote. Yesu alionya, hata hivyo, kwamba katika siku za mwisho watumishi mabaya wataingia ndani ya Kanisa kwa jitihada za kuweka Bibi arusi kulala. Wao watajaribu kumondoa moyo wake wa upendo anaopenda Bibi-arusi wake kwa kudai, "[Bwana] wangu anakawiya kuja" (24:48).

KILIO CHAKO HUSUKUMA MOYO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Neno la Mungu linashuhudia ukweli kwamba mateso hutufundisha kupiga magoti na kulia mbele ya Bwana katika shida zetu zote na matatizo yetu.

"Kabla sitajateswa mimi nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako" (Zaburi 119:67).

"Najua, hukumu zako ni za haki, Ee Bwana, na kwa uaminifu umenitesa" (119:75).

TUMAINI LENYE KUUZUNISHA

David Wilkerson (1931-2011)

"Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, na kwa sababu ya maovu yao, hijitesa." (Zaburi 107:17).

Kwa mujibu wa kamusi, mpumbavu ni mtu asiye na hukumu au fikila nzuri - mtu anayefanya makosa ya silly. Anafanya jambo lake mwenyewe bila kufikiria matokeo.

KUSHAMILI KATIKA HALI YOYOTE

Gary Wilkerson

"Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, furahini" (Wafilipi 4:4).

"Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hari yeyote niliyo nayo. Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu." (4:11-13).