WALIKUWA HURU NDANI YA TANURU!
Sisi sote tunajua hadithi vizuri. Mfalme Nebukadneza, mtawala wa Babloni, aliita kila kiongozi kutoka katika ufalme wake wa mbali ili kukusanyika pamoja ili waheshimu miungu ya uongo. Mfalme alijenga sanamu kubwa, dhahabu na kujaza viongozi wenye kuvaa mavazi ya kuvutia – wakuu wa majimbo, wana wa mfalme, mahakimu na maafisa wa majimbo - pamoja na watu wote wa nchi walipaswa kuzingatia amri ya mfalme na kuinama mbele ya sanamu. Je! Na kama hawangerifanya hivo? Ilikuwa ni hukumu ya papo hapo ya kifo.