Body

Swahili Devotionals

TAFUTA UONGOZI WA MUNGU

Nicky Cruz

Nilikuwa na myaka ishirini na mbili tu wakati Mungu aliweka moyoni mwangu mapenzi yake kwangu kuwa mhubiri. Aliniagiza kutumia historia yangu na ushuhuda wangu wa kusukuma wenye dhambi kwa wokovu, na tangu wakati huo nimebakia mwaminifu kwa wito huo. Wakati mwingine nimekuwa nimechoka kwa kuwaambia hadithi yangu, na nilipendelea Mungu anitumie kwa lengo lingine. Ni vigumu kufikisha kumbukumbu mara kwa mara.

KUPONYA NAFSI HII YENYE SHIDA

David Wilkerson (1931-2011)

Mchungaji kijana aliniita, alikuwa tayari kuacha huduma. Bwana alikuwa amemtumia kwa njia ya ajabu, lakini sasa alikuwa amevunjika moyo, akijisikia kuwa hana maana, hakuwa na faida kwa Mungu hata kidogo. Aliponiita, alipigwa na butwaa juu ya maamuzi fulani aliyoyafanya na alionyesha kwamba alikuwa tayari kuacha. Alikuwa na hasira kwa Mungu na wakati alipokuwa akizungumza nami, nilihisi kwamba alitarajia kuwa na hasira naye. Lakini alikuwa amevunjika moyo sana na kupigwa chini kwamba nilihisi upendo na huruma peke yake vya Mungu viwe juu yake.

SIRI YA UMOJA

David Wilkerson (1931-2011)

Katika Yohana 13, Yesu alichukua kitambaa na baseni na kuosha miguu ya wanafunzi wake.

"Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa nyinyi" (Yohana 13:14). Baada ya kuwatawadha miguu yao, akawauliza, "Je, mnajua kile nilichowafanyia?" Kwa maneno mengine, "Je, munaelewa maana ya kiroho ya kutawadhana miguu?"

Ninaamini wakati Yesu alitawaza miguu ya wanafunzi, alikuwa akifundisha somo la kina juu ya jinsi ya kupata umoja wa ushirika ndani ya Mwili wa Kristo.

KITU CHENYE THAMANI KUBWA KWA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

"Wewe uliyeteswa, uliyerushwa na tufani, usietulizwa, tazama, nitaweka mawe yako kwa rangi nzuri, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi. Nami nitaifanya minara yako ya akiki nyekundu, na malango yako ya almasi, na mipaka yako yote ya mawe yapendezayo. Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na Amani ya watoto wako itakuwa nyingi" (Isaya 54:11-13, Toleo la Bibilia ya Mfalme Yakobo (KJV).

FARAJA KATIKA HUZUNI

David Wilkerson (1931-2011)

Siri ya kuelewa jinsi Mungu anatuokoa kutokana na mateso yanaweza kupatikana katika kuelewa jinsi alivyookoa Israeli kutoka utumwa wao.

"Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi" (1 Wakorintho 10:11).

Kila kitu kilichotokea Israeli - utumwa wao, majaribio yao, ukombozi wao kutoka Misri - ni ushuhuda, sanamu na mifano kwa sisi leo. Hakika, ukombozi wa kimwili wa Israeli unawakilisha ukombozi wa kiroho tunawoona.

USHINDI WA MAISHA YENYE KUJAA FURAHA

Gary Wilkerson

"Furahini katika Bwana siku zote; tena nasema, furahini. Upole wote na ujurikane na watu wote. Bwana yukaribu. Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijurikane na Mungu. Amani ya Mungu ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. Hatimaye, ndugu zangu mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, tayafakarini hayo" (Wafilipi 4:4-8).

NENO LENYE UHAI

Carter Conlon

Tunaishi katika siku za mwisho na ulimwengu kama tunavyojua unaenda ndani ya giza isiyoonekana. Unabii wa Kibiblia unaonekana mbele yetu kila siku, na hivi karibuni tutaona Yerusalemu iliyozingilwa na majeshi.

Yesu alionya kwamba katika siku za mwisho, manabii wengi wa uongo watatokea na Wakristo wengi watapotoshwa (tazama Mathayo 24:11). Hebu niwaambie kwa nini watapotoshwa: Ni rahisi tu, kwa sababu hawaishi katika Neno la Mungu! Wanafuata vitabu, mitindo, na wasemaji wenye kutania - lakini hawafungui maandiko ya Biblia.

KUSHIRIKI KATIKA FURAHA YA MUNGU YENYEWE

David Wilkerson (1931-2011)

"Wapendwa, ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana" (1 Yohana 4:11). Upendo wa kila mmoja ulioelezwa hapa sio tu kushikana mkono, kumkumbatia haraka awo wakusifiana. Apana, aina hii ya upendo inaona haja ya mwingine na hufanya kitu juu yake. Kwa kweli, kulingana na Yohana, ikiwa tunamwona ndugu yetu akihitaji na tusifanye chochote, upendo wa Mungu hauko ndani yetu.