MUONGOZO KUTOKA KWA ROHO MTAKATIFU
Kusudi la Mungu kwa watoto wake ni kwamba tunajisalimisha kwa utawala na uzibiti wa Roho Mtakatifu: "Ikiwa tunaishi katika Roho, na tuenende pia katika Roho" (Wagalatia 5:25). Kwa maneno mengine, "Ikiwa anaishi ndani yako, wacha akuongoze!"
Wakristo wa kwanza hawakutembea katika machafuko, kwa sababu waliongozwa na Roho. Waliwasiliana na Roho Mtakatifu na yeye aliwaelekeza. Kutembea katika Roho kunamaanisha uwazi wa kusudi na kutowa uamuzi usio na kiburi.