Body

Swahili Devotionals

KUENDELEZA TABIA YA MAOMBI

David Wilkerson (1931-2011)

"Bali wewe unapoomba, ingia chumbani kwako, na ukisha kufunga mlango wako, omba kwa Baba yako aliye katika mahali pa siri; na Baba yako aonaye kwa siri, atakubariki kwa uwazi” (Mathayo 6:6).

Yesu anaposema juu ya kwenda mahali pa siri kumtafuta Baba, anasema juu ya kitu kikubwa sana kuliko kitu kinacho kuwa kalribu ya mwili. Anazungumzia mahali popote ambapo unaweza kuwa peke yake naye katika ushirika wa karibu.

MWENZI WA KILA WAKATI WOTE

David Wilkerson (1931-2011)

"Wakati Yeye, atapokuja huyo Roho wa ukweli, atawaongoza kwenye ukweli wote; kwa maana hatanena kwa ajili ya mamlaka Yake, lakini chochote atakachosikia atakinena; naye atawambia mambo yatakayokuja. Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atachukua kilicho ndani yangu na kukitangaza” (Yohana 16:13-14).

AMANI INAOSHINDA

Gary Wilkerson

"[Yeye] ametuokoa na kutuita kwa wito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu sisi,  bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake. Nema hiyo ambayo tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele" (2 Timotheo 1:9).

Kila mwamini ana wito wa juu kutoka kwa Bwana, na Mungu anaahidi kwamba ikiwa tutatenda kwa imani, tukimwamini, ataleta mpango huo kufanikiwa. Lakini kila mtu ambaye ametembea na Yesu kwa urefu wowote wa muda anaweza kushuhudia, kufuata wito wetu kunamaanisha tutakutana na vizuizi njiani.

KUSHINDWA SIO MWISHO

Tim Dilena

Petro ni mfano mzuri wa mwamini ambaye alishindwa na kisha akajikakamuwa na akafurahia mafanikio makubwa. Kabla ya kusulubiwa kwa Yesu alimkataa mara tatu (soma akaunti hiyo katika Marko 14:66-72). Wakati ambao alipata nafasi nzuri ya kumtukuza Kristo, yeye alimkataa kabisa. Lakini baada ya ufufuo, Petro alikutana na mtu mmoja-mmoja pamoja na Yesu ambaye ilimuekea maisha mapya na nguvu katika huduma yake.

UTAJIRI WA AJABU WA NEEMA YA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Maandiko yanasema, "Lakini kwake  ninyi mmepta kuwa katika Kristo Yesu, ambaye alifanywa kwetu kuwa hekima itokayo kwa Mungu, na haki na utakaso na ukombozi" (1 Wakorintho 1:30). Usitowe kwa maneno yote katika aya hii. Kwa ufupi, lengo la injili ni ukombozi na neema ya Mungu inajumuisha kila kitu alichotufanyia kupitia Kristo kwa kutukomboa kutoka kwa nguvu za shetani na kutuleta katika ufalme wa nuru yake tukufu!

KUTEMBEA KATIKA ROHO

David Wilkerson (1931-2011)

Mtume Paulo alisema, "Endeni kwa Roho, wala hamutatimiza kamwe tamaa za mwili" (Wagalatia 5:16). Alisema pia, "Ikiwa tunaishi katika Roho, na tuenende pia kwa Roho" (5:25).

Kutembea katika Roho ni kumruhusu Roho Mtakatifu kufanya ndani yetu kile Mungu alimtuma kufanya. Yesu alisema juu ya Baba, "Atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi milele – ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa sababu haumuoni wala haumjui; lakini ninyi mnamjua, kwa maana anakaa nanyi na atakuwa ndani yenu” (Yohana 14:16-17).

SIKILIZA ONYO HILO

David Wilkerson (1931-2011)

"Kuanzia mdogo wao hata aliye mkubwa miongoni mwao, kila mmja nimwenye kuwa na tamaa; na kutoka kwa nabii hata kwa kuhani, kila mtu anatenda uwongo… Je! waliona aibu wakati wamefanya machukizo? Hapana! Hawakuwa na aibu kamwe" (Yeremia 6:13, 15).

KUWEZESHWA NA ROHO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Wale ambao wanashikilia imani isiyo geuka, wako kwa udhihirisho mtukufu wa nguvu ya ufufuo wa Kristo. Ni wewe na Bwana tu ndio mtajua shughuli zote za karibu lakini atakushangaza; atakufurahisha; atakuonyesha utukufu wake!

Ukuu wa sasa wa Kristo unaweza kuangaziwa kwa kifungu kimoja cha nguvu: "Ndani yake ndimo kulikuwa uzima" (Yohana 1:4) Alikuwa - na sasa - ni mwenye nguvu ya maisha. Yesu alikuwa akigeuzwa kila wakati alipokuwa akichota kwenye hifadhi ya siri ambayo haikumalizika. Yeye hakuchoka na umati wa watu ukimshinikiza na uvumilivu wake haukuvaa  kukonda.