Body

Swahili Devotionals

JE! UNAAMINI KWAMBA MUNGU AKIKUPITIA ATAKUONA?

David Wilkerson (1931-2011)

Swali muhimu zaidi linalowakabili watu wa Mungu katika siku hizi za mwisho ni hili: "Je! Unaamini kwamba Mungu atakuona akikupitia? Je! Unaamini kuwa anaweza kufanya yote yanayotakiwa kujibu maombi yako na kukidhi mahitaji yako?" Hili ndilo swali moja ambalo Bwana wetu aliwauliza wale vipofu wawili ambao walimwomba rehema na uponyaji. "Je! Mnaamini kwamba ninaweza kufanya hili?' Wakasema, 'Ndio, Bwana.'… Na macho yao yakafunguliwa” (Mathayo 9:28-30).

KUHUSIANA NA WATU WA MUNGU

Gary Wilkerson

"Namshukuru Mungu wangu kira niwakumbukapo ... kwa sababu ya ushirika wenu katika kuieneza injili tangu siku ya kwanza hadi sasa" (Wafilipi 1:3-5).

Paulo anamshukuru Mungu kwa ushirika wa watakatifu; koinonia - kushiriki pamoja - ambao yeye na kanisa la Wafilipi walifurahia wakati walikua wanatembea pamoja kwa imani. Ushirika huu katika injili sio kama mwingine wo wote. Una nguvu kwa sababu umezaliwa chini ya msalaba wa Yesu Kristo. Kupitia yeye, kupitia wanaume wa sehemu mbali mbali, makabila, na lugha zote hukutana kama mwili mmoja.

LEO MAMBO YOTE YANAWEZEKANA KWA MUNGU

Carter Conlon

Baada ya kifo cha kaka yao, Maria na Martha walikuwa na huzuni. Lazaro alikuwa amekufa kwa siku nne na umati mkubwa wa waomborezi ulikusanyika wakati Yesu alipofika. Maria alianguka mbele ya miguu wakati alipomwona, na wakati Yesu alimwona yeye na wengine wakilia, "aliomboleza ndani ya roho na kufadhaika" (Yohana 11:33). Kumbuka kwamba Lazaro na dada zake walikuwa marafiki wa karibu na Yesu, na walikuwa wakimpekea nyumbani kwao mara nyingi. Hata hivyo, baada ya ndugu yao kufa, dada hao hawakuonekana kuwa Yesu anaweza kufanya muujiza.

KWENDA MBALI UKIWA PAMOJA NAYE

David Wilkerson (1931-2011)

Ufunuo mkubwa zaidi ambao wanafunzi walikuwa hajawahi kuupata ulikuwa unazingatia ufufuo wa Yesu Kristo. Ilikuwa siku ya kwanza ya juma, na wanafunzi walikuwa wamejificha nyuma ya milango imefungwa kwa ajili ya kuogopa Wayahudi. Ghafla, Yesu alionekana - katika utukufu kamili wa ufufuo - kushinda kifo, kuzimu, na shetani. Aliwaonyesha wanafunzi mikono yake, miguu yake, upande wake uliovunjwa, halafu akawajaza na kusema, "Pokea Roho Mtakatifu" (Yohana 20:22).

ALIJITOWA KWA UPENDO WAKE

David Wilkerson (1931-2011)

"Mungu, atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake " ... kwa wale wenye fitina, wasiotiie ukweli, bali wakubalio dhuluma, watapa hasira na ghadabu; dhiki na huzuni juu ya kila nafsi ya mtu anayefanya uovu , Myahudi kwanza na Mugiriki pia; bali utukufu na heshima, na amani kwa kila mtu anayefanya mema." (Warumi 2:5-6, 8-10).

ARDHI TAKATIFU YAKO MWENYEWE

David Wilkerson (1931-2011)

Mungu alipomwita Musa kutoka kwenye kichaka kilichowaka, akamwambia: "Vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali unaposimama ni patakatifu" (Kutoka 3:5). Nchi takatifu si sehemu ya kimwili, lakini ni ya kiroho. Wakati Mungu alimwamuru Musa kuvua viatu vyake kwa sababu alikuwa kwenye ardhi takatifu, hakuwa akizungumzia kwa njma nne kwa mbili za mali yake inayoonekana. Alikuwa akizungumzia hali ya kiroho.

KUNG’AA SANA KWA AJILI YA KRISTO

Gary Wilkerson

"Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii siku zote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa Zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake njema" (Wafilipi 2:12-13).

Barua ya Paulo kwa Wafilipi imejaa sifa, faraja, na baraka. Anavutiwa na kutembea kwao kwa utii, na anawasifu kwa kuwa rahisi sana kushirikiana nao. Anawasifu pia kwa kuwa imara na kutoyumbayumba hata wakati yeye hayupo hapo kwa kuwaongoza.

KUFUNA KATIKA MAFUNZO YAKO YAKO

Tim Dilena

"Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa Imani yenu huleta saburi. Na muache saburi  iwe na kazi kamilifu, mpate  kuwa wakamilifu bila kupungukiwa na neno. Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe Mungu" (Yakobo 1:2-5).

KUWEZESHWA NA UWEPO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Maandiko hutoa mifano isiyo na mwisho ya jinsi uwepo wa Bwana huwawezesha watu wake kuishi kwa ajili yake. Chukua Musa, kwa mfano, aliamini kwamba bila uwepo wa Mungu katika maisha yake, ilikuwa ni bule kwake kujaribu jitihada yoyote. Alipokuwa akizungumza uso kwa uso na Bwana, alisema kwa ujasiri, "Ikiwa Uwepo wako hauendi pamoja nasi, usituchukuwe kutoka hapa" (Kutoka 33:15). Alikuwa akisema, "Bwana, ikiwa haundi nasi, hatuwezi kufanya hivyo. Hatuwezi piga hatua hata moja bila uhakika wa uwepo wako."