Body

Swahili Devotionals

​IBADA INAYOTAKINA KWA MUNGU WETU WA KUSHANGAZA

Gary Wilkerson

Maandiko yamejaa tahadhari juu ya kuleta ibada yenye kuwa bule mbele ya Mungu. Ikiwa kanisa leo linafikiri mambo mazuri, kujisaidia na kufanya watu kujisikia vizuri, kisha wanamitindo wa kiroho wa kisasa kama Tony Robbins au Oprah Winfrey inaweza kukamilisha hili kwa ajili yetu. Lakini kanisa sio juu ya kile tunaweza kufanya; ni kuhusu kile Kristo anaweza kufanya.

WEKA JAMBO HILO KWA MKONO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Yesu alisema, "Yeyote asiyechukua msalaba wake na kunifuata, hanistahili" (Mathayo 10:38). Na pia, "Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, na ajitwike msalaba wake, anifuate" (Mathayo 16:24). Paulo pia alitangaza, "Lakini Mungu alikataza hilo, ili nisione fahari ya juu ya kitu cho chote ila msalabani wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulubishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu" (Wagalatia 6:14).

VITA VYA SHETANI DHIDI YA KANISA

David Wilkerson (1931-2011)

Kitabu cha Ufunuo kinatuambia kwamba katika siku za mwisho, Shetani atafufuka kwa ghadhabu na kupigana vita "na mabaki." Bila shaka, mabaki hayo ni Mwili wa Kristo, unaohusishwa na wote "wanaozingatia amri za Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo" (Ufunuo 12:17).

Sisi katika kanisa la Kristo tunaongea mara nyingi juu ya mapambano ya kiroho; Vita vinavyoelezewa katika Ufunuo ni mashambulizi ya duniani kote amabayo Shetani ameanzisha dhidi ya Mwili wa Kristo: "Alipewa nafasi ya kupigana na watakatifu" (13:7).

BWANA HUPENDA KANISA LAKE

David Wilkerson (1931-2011)

Ayubu anauliza, "Je! Mtu ni nini, hata ukamtukuza, na kumtia moyoni mwako, na kumwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?" (Ayubu 7:17-18).

Waebrania 12:1 inatuambia kwamba ulimwengu umezungukwa na wingu la mashahidi ambao wako pamoja na Kristo katika utukufu. Je! Hii wingu kubwa inashuhudia - na ushahidi wao una maanniisha ? Wanaongea na kizazi chetu, kupitia maisha yao na maneno yao kama ilivyoandikwa katika Maandiko. Ninaamini wanasema mambo matatu kwetu:

ONGEZEKO LA UWEPO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Mungu anafanya jambo jipya katika kanisa lake leo. Kazi hii kubwa ya Roho haiwezi kupatikana katika eneo moja. Inatokea ulimwenguni pote, ndio, hauitaji kufanya safari ya mbali ili uyikumbatiye. Hakika, "kitu kipya" cha Mungu kinaweza kuwa karibu kama kanisa lilivyo karibu.

KUPENDANA KWA UJASILI KAMA YESU ALIVYOFANYA

Gary Wilkerson

Tunapochunguza maisha yetu kama wafuasi wa Yesu, wengi wetu hafwaati mfano wa Agano Jipya. Kristo aliwatuma wanafunzi wake kumi na wawili kuitangaza habari njema, kuponya wagonjwa, na kuwa tayari vyombo vya kuleta ufalme wake duniani (angalia Marko 16:15-18). Baadaye, aliwatuma wanafunzi sabini na maagizo sawa (angalia Luka 10:1-16). Aliwaambia kila mmoja wa makundi haya, "Kila kitu niliowafundisha kufanya - kuhubiri injili, kuponya wagonjwa na kuleta ndani ya ufalme wangu - munapaswa kufanya hayo kwa jina langu. Sasa nenda ulimwenguni pote na mufanye kama nilivyoamuru."

UPWEKE UKO MAHALI POTE

Nicky Cruz

Tunahitaji kutofautisha kati ya kuwa mwenyewe, upweke na kutengwa. Kuwa mwenyewe, ni hali ya kujitenga na watu wengine. Wakati mwingine familia, marafiki na watu wengine kwa kutopatikanan mbele yetu, lakini tu kwa sababu sisi tuko wenyewe haimaanishi sisi tuko kwenye upweke. Tunachukua tu nyakati hizi kwa kuzingatia na kutambua kuwa maisha haiwezi kujazwa na watu daima.

KUJIANDAA KWA SIKU ZIJAZO

David Wilkerson (1931-2011)

"Siku ya Bwana itakuja kama mwizi usiku" (2 Petro 3:10). Mungu hutumia watumishi waaminifu - wakati mwingine wale wenye vurugu za kitaifa na wakati mwingine wanyenyekevu, wasiojulikana, walinzi wa siri - kutoa maneno yake ya onyo. Ni wale tu ambao hawapendi dunia hamu sana ya kuja kwa Bwana kwa kuwa atawalete ujumbe wa kweli katika mioyo yao.

​MUNGU AMESHIKILIA NENO LAKE

David Wilkerson (1931-2011)

Ujasiri katika sala hutoka kwa kuwa na ujuzi wa kitu kinachoitwa "kushikilia kipaumbele." Ikiwa unaweza kuelewa ukweli huu, utabadili milele namna yakuomba. Mfano ni "kesi iliyotangulia" ambayo hutumika kama mfano katika kesi zifuatazo. Na "kushikilia kipaumbele" ni uamuzi wa kisheria uliofanywa zamani ambao unakuwa utawala wa mamlaka kwa kesi sawa za baadaye. Kwa majaji, hii inamaanisha kusimamia uamuzi uliofanywa tayari.

UNAKWENDA WAPI UNAPOKABILIWA NA SHIDA?

David Wilkerson (1931-2011)

Unaweza kufurahia msimu wa nyakati nzuri sasa - hakuna shida kubwa, majaribio ya kukata tamaa au maumivu makubwa. Ninamshukuru Bwana kwa kutoa nyakati hizo katika maisha ya watoto wake. Lakini tunajua kutoka kwa Maandiko kuwa dhoruba na majaribu makubwa hatimaye huja kwa wote ambao wametowa kwa ukweli kila kitu kwa Kristo. "Mateso ya mwenye haki ni mengi, lakini Bwana humponya kutoka yote" (Zaburi 34:19).