ALIAHIDI KWA KIAPO CHA MILELE
Katika sala ya Yesu kwa Baba, anasema: "Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, name naja kwako. Baba Mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo" (Yohana 17:11). Alikuwa akisema, "Tulikubaliana kwamba nitaweza kuleta agano letu kwa kila mtu anayeniamini. Sasa, Baba, nakuomba kuwaleta wapendwa hawa chini ya ahadi ile ile ambayo umeniahidi."