Body

Swahili Devotionals

​ALIAHIDI KWA KIAPO CHA MILELE

David Wilkerson (1931-2011)

Katika sala ya Yesu kwa Baba, anasema: "Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, name naja kwako. Baba Mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo" (Yohana 17:11). Alikuwa akisema, "Tulikubaliana kwamba nitaweza kuleta agano letu kwa kila mtu anayeniamini. Sasa, Baba, nakuomba kuwaleta wapendwa hawa chini ya ahadi ile ile ambayo umeniahidi."

ISHARA ZA KUJA KWA KRISTO

David Wilkerson (1931-2011)

"Wakati mwasema, kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, hakika hawataokolewa. Bali ninyi ndugu, hammo gizani hata siku ile iwapate kama mwivi" (1 Wathesalonike 5:3-4).

MBELE YA KITI CHA BABA

David Wilkerson (1931-2011)

Watumishi wa Mungu wanapaswa kuja mbele yake kikamilifu wakiamini kwamba atajibu. Ni jambo nzuri kuleta ahadi za Mungu katika sala pamoja na wewe – kwa kusimama kama unamkumbusha. Hakika, hapotezi fahamu yakukumbuka, lakini Bwana anatupenda sisi kwa kuleta ahadi zake mbele yake.

​KUSUBIRI SIKU YA UTUKUFU

David Wilkerson (1931-2011)

"Msifadhaike mioyoni mwenu; amini Mungu, na mimi pia muniamini. Nyumbani kwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningeliwambia; maana naenda kuwaandalia mahali kwa ajili yenu" (Yohana 14:1-2).

Wengi wetu wamehamisha hesabu ya mida kupitia maisha yetu,  lakini wakati tutapofika mbinguni, hatutahama tena. Yesu anatuambia kwamba amekwenda kutuandalia mahali na ni nyumba ya kudumu. Mwanamke Mkristo aliuliza, "Ikiwa mbinguni kutakuwa mengi asiewezekana kuhesabiwa, Mungu atawezaje kufanya makawo ya kila mtu? Inawezekanaje kuwa na nafasi ya kutosha kwa maeneo mengi?"

GIZA HALIWEZI KURUDIA BILA MAPAMBANO

Carter Conlon

Wakati wowote Mungu atakapofanya kitu kikubwa, watu wake watakuwa na upinzani kinyume chake. Mtume Petro alisema hivi: "Wapendwa, msifikiri kuwa ni ajabu uyo msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwambwa ni kitu kigeni kiwapatacho. Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe " (1 Petro 4:12-13).

KUTAFUTA MAPUMZIKO KATIKA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Shetani anapenda kusema uongo kwa watoto wa Mungu. Analenga wale ambao wameamua kuingia katika mapumziko ya Mungu aliyoahidiwa. "Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu. Kwa maana yeye aliyeingia katika mapumziko Yake amestarehe mwenyewe katika kazi zake kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake. Basi, na tufanye bidii kuingia katika pumziko hilo, ili kwamba mtu yeyote asije akaanguka kwa mfano huo wa kuasi" (Waebrania 4:9-11).

USALAMA WETU KAMA WATOTO WA MUNGU

David Wilkerson (1931-2011)

Yesu alimwita Roho Mtakatifu "Msaidizi." "Rakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, yeye ambaye Baba atamtuma kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliowaambia" (Yohana 14:26, KJV). Ni jambo moja kumjua Roho Mtakatifu kama Msaidizi wetu, lakini pia tunapaswa kujua jinsi anatufariji ili tuweze kutofautisha faraja gani ya mwili na yale ya Roho.