YESU TAYARI ANATAWALA KAMA MFALME!
Nebukadneza akaweka sanamu ya ngo’ombe ya dhahabu huko Babiloni na akaomba iabudiwe. Kila afisa, kila kiongozi na kila raia katika mikoa mia moja ya Babiloni walipaswa kuanguka chini mbele ya mungu huu au kukabiliana na kifo – kwa kuchomwa hai ndani ya tanuru. Hata hivyo, Wayahudi watatu waaminifu katika ufalme walikataa kuinama, na mfalme akawa na hasira na akawatupa kwenye tanuru la moto.