JE! UNAJISIKIA KUWA HAUFAI NA KUWA NA MISUKOSUKO?
Ikiwa umewahi kuwa na nyakati za kujisikia kama haufai na kuwa na misukosuko, basi Zaburi 77 iliandikwa kwako. Mwandishi wa Zaburi hiyo, mtu mmoja aitwaye Asafu, alikuwa Mlewi kutoka kwenye ukoo wa makuhani huko Israeli. Alikuwa pia mwimbaji na aliwahi kuwa mkurugenzi aliyechaguliwa na Daudi. Kwa ujumla, Asafu aliandika Zaburi kumi na moja na zilikuwa zimejaa mafundisho ya haki kwa watu wa Mungu.