KABLA YA KUUMBWA, MUNGU ALIKUWA ANAKUJUA
Kulingana na Yesu, kwa macho ya Mungu Kristo na Kanisa lake ni moja. Paulo anaonyesha hili kwa mfano wa mwili wa mwanadamu. Anasema Kristo ndiye kichwa na sisi ni mwili wake - mfupa wa mfupa wake, nyama ya mwili wake. "[Mungu] akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa, amabalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote" (Waefeso 1:22-23). "Kwa maana sisi ni viungo vya mwili wake, wa mwili wake na mifupa Yake" (Waefeso 5:30).